by Sunday Shomari
Dotto Mwaibale, Morogoro
WAANDISHI wa Habari nchini wametakiwa kutumia taaluma yao kwa ajili ya kuhamasisha Umma kuhusu umuhimu wa Takwimu.
Wito huo umetolewa na Mkurugenzi wa Takwimu za Kiuchumi Morice Oyuke kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Dkt. Albina Chuwa.mjini Morogoro leo asubuhi wakati akifungua Warsha ya siku moja ya kuwajengea uwezo wanahabari kuhusu namna bora ya kuandika habari za kitakwimu.
“Ninyi wanahabari ni muhimu katika masuala ya takwimu hivyo ni vizuri mjifunze jinsi takwimu zinavyoisaidia serikali, wadau wa maendeleo na wadau wa takwimu katika kupanga Sera na kufanya tathmini ya utekelezaji wa mipango mbalimbali ya kitaifa na kimataifa kama vile Dira ya Taifa ya Maendeleo ya mwaka 2025 Tanzania Bara na mwaka 2020 Tanzania Zanzibar” alisema Oyuke.
Oyuke alitaja mambo mengine wanayopaswa kujifunza ni Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umaskini Tanzania Bara (Mkukuta) Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umaskini Zanzibar (Mkuza) na Mpango wa Taifa wa Maendeleo wa Miaka Mitano 2010/11 mpaka 2015/16 na Malengo ya Melenia (MDGs)
Alisema eneo jingine watakalofundishwa ni kuhusu Pato la Taifa na jinsi linavyokokotolewa na bei za ajira, takwimu za jamii na umuhimu wake.
Dk.Chuwa alisema vyombo vya habari vinajukumu la kutoa taarifa sahihi zilizo rasmi ambazo zinazalishwa na tafiti mbalimbali nchini ili ziwafikie wadau wote nchini bila ya kupoteza maana.
sunday Shomari | JTarehe 22, Mwezi wa Sita 2014
| URL:http://wp.me/pYraF-dcS
Comment
See all comments
Unsubscribe to no longer receive posts from Sundayshomari’s Blog.
Change your email settings at Manage Subscriptions.
Trouble clicking? Copy and paste this URL into your browser:
http://sundayshomari.com/2014/06/22/warsha-ya-kuwajengea-uwezo-wanahabari-kuhusu-uandishi-wa-habari-za-kitakwimu-yafanyika-mkoani-morogoro/